DARASA LA ALHAMISI na DR. CHRIS MAUKI: IFAHAMU MISONGO YA MAWAZO INAYOTATIZA FAMILIA NYINGI (FAMILY STRESS). PART 2



za kukuonyesha kuwa misongo ya mawazo ipo ndani ya familia
  • Mahusiano nje ya ndoa
  • Muda mwingi kazini hata kama hakuna kinachofanywa huko
  • Malumbano kuzidi
  • Mmoja kutokuwa tayari kumhudumia  mwenzake katika tendo la ndoa    “sexual withdrawal”
  • Kuanza au kuzidi kwa matumizi ya vilevi
  • Hali ya mmoja kupooza na kukosa raha wakati mwingi
  • Uadui baina ya wanandoa

Matokeo ya kuzidi kwa dalili hizi
  • Talaka au kutengana
  • Mmoja kunyanyasika au wote kunyanyasana
  • Unyanyasaji wa watoto( child abuse) nk.

Visababishi toka nje ya familia(extrafamily stressors)
  • Kazi
  • Mahangaiko ya maisha
  • Familia kubwa(extended family)
  • Kukosa kazi
  • Mshahara mdogo kazini
  • Matatizo ya shule(hasa kwa wale wanaosoma wakiwa ndani ya ndoa)
  • Kukosa elimu(kwa wale ambao hawakubahatika kusoma)

Matokeo ya misongo hii kiafya baina ya wanandoa
  • Kuongazeka kwa matatizo ya shinikizo la damu
  • Kuongezeka kwa matatizo ya misuli(muscle tention)
  • Kuongezeka kwa mapigo ya moyo
  • Kuongezeka kwa kasi ya mfumo mzima wa upumuaji(breathing system)

Hali hii inapozidi kwa wanandoa tunategemea yafuatayo
  • Magonjwa ya moyo
  • Shinikizo la damu
  • Vidonda vya tumbo( ulcers)
  • Maumivu makali na ya mara kwa mara ya kichwa
  • Maumivu ya mara kwa mara ya mgongo
  • Hypertension
  • Saratani (cancer)
  • Hofu kubwa katika baadhi ya vitu( allergic reaction)

Msongo wa mawazo juu ya masuala ya uzazi wa mpango
Pangeni ninyi wawili kukutana na kuzungumza na mshauri, hili sio jambo la mmoja wenu bali wote. Fanyeni chaguzi fasaha ni njia ipi ya uzazi wa mpango mtaiweza na mtaipenda. Tafuteni taarifa Muhimu za kuhusu uzazi wa mpango toka kwa wataalamu, marafiki, ndugu, vitabu, na vijarida husika, msitegemee taaria za uzushi zisizoweza kuaminika.

Yamkini njia nyingine zitakinzana na imani au misimamo yako binafsi, basi pata ushauri toka kwa kiongozi wako wa dini. Katika kuyatimiza haya yote shirikianeni kwa upendo katika kuelekezana na kukumbushana  juu ya ushauri mlioupata.

Msongo wa mawazo unaosababishwa na mzazi mmoja kuwa mbali na familia
Panga kuitembelea familia yako kila upatapo nafasi zaidi ya kwenda maeneo mengine. Wasiliana nao kwa simu  mara kwa mara, hii inaruhusu  muda wa maongezi na kujuliana hali. Njia nyingine isiyo ya gharama sana ni kutumiana barua, hapa ninatia msisitizo katika barua na sio kadi. Kadi kama za siku za kuzaliwa na nyingine hazina uzito mkubwa wa mawasiliano kama ule uliopo katika barua. Lazima familia yako ijue kuwa unatumia jitihada zako zote katika kuwasiliana nao hii itawajengea haja moyoni ya kutaka kukujibu.

Misongo ya mawazo inayoletwa na masuala ya fedha
Stress zinazosababishwa na masuala ya fedha ni mbaya sana, zaweza kuvunja mahusiano baina ya wanafamilia, zaweza kuleta matatizo kiafya hasa pale matibabu yanapocheleweshwa mpaka mgonjwa azidiwe sana kwasababu ya ukosefu wa fedha. Hali hii huwafanya wanafamilia kuwa na hisia mbaya, kutojithamini, na  kutojipenda, hali ya kujitawala kwao hushuka maana hamna mwenye uhakika na maisha.

Jinsi ya kukabiliana na misongo hii.
Jifunzeni kuwa na bajeti ya mapato na matumizi ya familia, bajeti hii itawasaidia kupunguza madeni, ambayo kama yasipolipwa huleta stress zaidi na maranyingine kushitakiwa kisheria. Bajeti pia itawasaidia ninyi kutawala fedha zenu zaidi ya fedha  zenu kuwatawala ninyi.

Namna nzuri ya kuandaa bajeti ni kupiga picha nyuma, nijinsi gani mlitumia fedha mwakajana, au mwezi uliopita. Angalia vyanzo vyenu vya mapato, vile vikubwa na vile vidogovidogo. Wakati wote jitahidi sana matumizi yasije yakawa ya kasi kubwa kuliko kasi ya kuingiza. Fahamu ni vitu vipi hutumia fedha zenu zaidi, matumizi haya yawe ya lazima na yakishatimizwa yote ndio mwaweza kufikiria matumizi mengine ya anasa.  


Share on Google Plus

About Baraka Kiranga

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment