§ Kamwe kusiwepo na dharau baina yenu, mmoja asimdharau mwingine kwa chochote.
§ Unachotaka kutendewa, kuwa tayari kumtendea mwenzako tena kwa furaha na upendo.
§ Usafi uongezeke baina yenu, sio tu kwenye maeneo ya nje tu bali kwenye miili yenu pia
§ Mavazi na mikao yenu “pose” iwe ya kuhamasisha tendo la ndoa nasio kukatisha tama, hapa wanawake wanahusika zaidi.
§ Kuweni tayari kujifunza na hata kugharamia mazingira husika ili kuongeza hamasa zihusuzo tendo la ndoa.
§ Miili yenu na muonekano wa kila mmoja wenu uwe wa kuvutia na kuhamasisha tendo la ndoa na sio wa kukatisha tamaa katika zoezi hili, hapa namaanisha ukubwa wa mwili, uzito wa mwili na kitambi. Vitambi na miili mikubwa sana ni tatizo katika kulifurahia tendo la ndoa kwa wengi (hapa hakuna cha kujitetea, ukweli ndio huo)
Hii ni sehemu ya kwanza, usikose kumalizia muendelezo wa points hizi hapo kesho, karibu tujifunze wote, mkaribishe na mwenzako pia.

0 comments:
Post a Comment