BAADA YA KUONA MAANDALIZI NA UONGOZAJI WA SIKU YA MSANII ILIYOFANA PALE MLIMANI CITY HALL SASA CHUNGULIA BAADHI YA MATUKIO YALIYOKUWEPO

 Street dancers ikiongozwa na Super Nyamwela, jamaa walitishaaaa

 MC Dr. Chris Mauki na Jokate Mwengelo ndio walikuwa washika mpini kuiongoza shuhuli nzima, Thanks to Haakneel production for this platform

 Mkurugenzi mtendaji wa Haalneel production Mr. Emmanuel Mahendeka akikabidhi hotuba yake fupi kwa mgeni wa heshima Makamu wa Rais Mh. Dr. Mohamed Gharib Billal

 Kaimu katibu mkuu mtendaji wa BASATA akiongea

 Naibu waziri wa Habari, utamaduni na michezo Mh. Juma Nkamia akiongea
 Ngoma kutoka Ukerewe ilibamba sanaaaaa,

 Isha mashauzi na vijana wake walitumbuiza vema pia

 Vijana toka Ako Mpiluka band nao walifanya manjonjo ya hatari, hapa wakicheza na moto, na picha ya chini ni sarakasi mahiri

 Diamond Platinums na kundi la wasafi waliweka alama ya tofauti kwenye jukwaa

 Nyomi ya watu wakifuatilia kila tukio jukwaani, huku mbele ni VIP's na nyuma ni IP
Wana Njenje, namwona kaka Kitime akigonga masauti

 Fashion show pia ilibamba sanaa na iliratibiwa na mama wa mitindo Asiah Hidarus, huyu ni rafiki yangu Mc, Zipompapompa na alivishwa na Asia Hidarus

 Huyu dada kama unamkumbuka aliwahi kuwa Miss Tanzania (Enzi hizo kabla hawajaanza kudanganya umri)

 Mama wa mitindo Asia Hidarus na wanamitindo aliowavisha, Zipompa kwa chati

 Kama kawa, nikiwa makini zaidi kuongoza tukio wakati huu mwenzangu Jokate akiwa anahoji watu Back stage, Thanks to my director Madudu, you really worked hard to make this thing a success, Mr Man you are good
 All the way from Nairobi Kenya, The Omondi's brothers, Eric na Fred Omondi wali crack mbavu za watu mbayaaaaa

 Vijana wa gumzo, Yamoto band, walisawazisha kila kitu madogo hawa, yani basi tu,
Mkurugenzi mtendaji Haakneel Production Mr. Mahendeka akiwa na Kaimu katibu mkuu BASATA, hawa wote wanavyopendeza walivukwa na dadangu wa ukweli Veronica chini ya LARENA Fashions, Big up and keep it real Veronica

Shukrani na pongezi za nguvu kwa chama kubwa, chama la ukweli lililovamia fani hii ya maevent kwa kasi na nguvu ya roketi----Haakneel production, kiukweli mmeweka standards za juu, you all deserve a clap and a hug. Big up sanaaa
Share on Google Plus

About Baraka Kiranga

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment