Ni mara nyingi sana na kuna uwezekano mkubwa sana kwa mwanaume kuona, kufikiri, au kudhania kuwa ndoa au mahusiano yake yako sawa kabisa na hayana tatizo lolote, tena anaweza kujigamba na kujisifu kabisa kwa hilo, wakati kwa upande mwingine mke wake anajisikia uchungu moyoni mwake na kukiri kwamba ndoa yao inawaka moto na yamkini mwanamke huyu anatamani hata watengane. Yako mambo madogo madogo sana kwenye mahusiano wanaume huyafumbia macho au kutokuyaona umuhimu wake kabisa huku wakidhani hali ni shwari, kinyume chake wake zao wakiyaangalia mambo hayo wanatamani ndoa ipasuke ili wapate pumziko. Labda umewahikuona ndoa nyingine kila kitu kinaonekana kiko sawa, mke na mume kwa nje mambo shwari wanaishi pamoja kwa miaka mingi tu na ghafla unasikia wametengana, halafu unashangaa nini kimetokea. Hapa inamaana mwanandoa mmoja kabanwa pumzi muda mrefu sana bila mwenzake kufahamu uhalisi wa maumivu ya mwingine. Hii imenifanya kujifunza kuwa, mtu sahihi wa kumuuliza hali ya ndoa au mahusiano (kama yanafuraha au kama yanamachungu) sio mwanaume bali ni mwanamke – Chris Mauki.
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)

0 comments:
Post a Comment