1. Peaneni uhuru wa kuwafanya muwe halisi na kuruhusu vipaji na vipawa vyenu kutenda kazi.
2. Mahusiano yenu yawe kwenye msingi wa penzi na sio kutawalana au kumilikiana.
3. Penzi na heshima vitawale zaidi ya nani anakipato gani na uwezo gani.
4. Wote muwe na jukumu la kuwezeshana, sio mmoja ndio wa kumwezesha mwenzake tu.
5. Kuweni marafiki wa kweli kabla hata ya kuamua kuwa wanandoa wa kweli.
6. Jifunzeni kufikiri na kuwaza kwa mtazamo wa “sisi’ na “vyetu” na sio mtazamo wa “wewe”, “mimi”, na “ changu” au “vyangu”.

0 comments:
Post a Comment